Wednesday, February 11, 2015

WATOTO WA MITAANI NA JINSI YA KUWASAIDIA Ukatili dhidi ya watoto umeongeza idadi ya watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi licha ya kuwepo juhudi za kupambana na tatizo hilo. Watoto wanaoishi katika mazingira hayo, huathirika kisaikolojia kutokana na kujiingiza katika vitendo vya matumizi ya gundi na dawa za kulevya, huku sehemu ya jamii katika ngazi ya familia na kuficha tatizo badala ya kulipeleka kwenye vyombo vya dola. Wanafanya hivyo kwa maelezo kuwa wanaogopa aibu, matokeo yake kuna ongezeko la watoto wa mtaani, baadhi ambao bado wapo chini ya matunzo ya wazazi wao, lakini wanajiingiza katika tabia ya kuomba fedha na wanaonekana mitaani katika miji mbali mbali nchini. Ukatili unafanyika dhidi ya watoto kuanzia ngazi ya familia na ndugu wa karibu kwa kumbaka au kumlawiti mtoto anyeishi nao. Sheria ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009, inalenga kurekebisha na kuimarisha sheria zote zihusuzo watoto, kuainisha haki, kukuza na kulinda maslahi bora ya watoto kwa mujibu wa sheria. Kuna uwezekano wa kulitokomeza hili tatizo la watoto wa mitaani, iwapo jamii itaamua kulichukua na kulipa nafasi kubwa na mikakati madhubuti katika kulitokomeza. Kutokana na furusa zilizopo kwa nchi yetu, kuwapatia hawa watoto shilingi mia au mia tano sio njia sahihi ya kulitokomeza tatizo la watoto wa miataani. Kuna uwezekano wa kuwapatia hawa watoto elimu ili mwisho wa siku na wao pia waweze kujitegemea badala ya kuwapatia mia tano ambayo wataitumia kwa mlo mmoja na tatizo linabaki palepale. Pia kutokana na vipaji mbalimbali walivyonavyo hawa watoto kuna uwezekano wa kuwaendeleza kwa vipaji walivyonavyo ili kwa vipaji hivyo viweze kuwasaidia maishani na waweze kuyaendesha maisha yao wenyewe badala ya kushinda barabarani wakiomba misaada.

Tuesday, February 10, 2015

KWA UFUPI Kutoka na changamoto hizo idadi ya watoto waishio katika mazingira magumu nchini wamekuwa wakiongezeka kila kukicha, huku vituo vya kuwahifadhi pia vikiongekezeka mfano wa maduka ya kuuzia vocha za simu.